Social Icons

Loading...

Maaskofu wa Makanisa ya Kipentekoste Watoa Tamko kuhusu vurugu za Mbagala.

TAMKO LA BARAZA LA MAASKOFU  WA MAKANISA YA KIPENTEKOSTE
TANZANIA (PCT)
Tarehe 25/10/2012
Ndugu wapendwa Wakristona Watanzania wenzetu kwa ujumla,tunawasalimu katika Jina la Bwana WetuYesu Kristo.Itakumbukwa kuwasikuyaterehe 12/10/2012 sote tulishitushwa na ghasia za kuchomwa kwa makanisa, Biblia Kuchanwa, kupigwa watumishi wa Mungu, kubomolewa kwa makanisa na sehemu takatifu za ibada yaani madhabahu kukojolewa;uhalifua mbao ulifanyika huko Mbagala jijini Dar es Salaam.
Pamoja na juhudi za Serikali yetu kupitia Jeshi la Polisi kufanya kazi ya kurejesha amani na utulivu Nchini, sisi .Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Kipentekoste tumesikitishwa na kitendo cha watoto waliohusika na kitendo cha kukojolea Quran (mtotowa Kikristo aliyekojolea Juzuu pamoja na mwenzake wakiislamu aliyemchochea kufanya kitendo hicho);pia tumehuzunishwa na kufadhaishwa zaidi baada ya kusikia tamko la serikali kupitia kwa waziri wa mambo ya ndani kuwa waliohusika na uvunjaji wa makanisa ni wahuni.
Kwa mtazamo wetu kama viongozi wa dini tunaona kauli ya serikali inamaanisha kuwa, SerikaliHaiamini kwamba waliohusika na uvunjaji wa makanisa,kuchoma Biblia,kubomoa na kukojolea madhabahu,kunywa na kula mikate ya meza ya BWANA pamoja na kuwapiga watumishi wa Mungu ni wanaosadikiwa kuwa ni wanaharakati wa kidini;bali ni
Wahuni tu.Kimsingi, utafiti uliofanywa na baraza letu unaonyesha kuwa vitendo hivi havikufanywa na wahuni bali wanaharakati wakidini
Kwa sababu zifuatazo:-
1. Mkusanyiko wa watu waliofanya uhalifu katika makanisa ulianzia msikitini baada ya sala ya adhuhuri, ukaelekea katika kituo cha Polisi ambapo mtuhumiwa wa kukojolea Juzuu alikuwa amehifadhiwa, na wakataka wapatiwe(kijana huyo anayetuhumiwa) ili wamwadhibu kwa mujibu wa sharia’h za kiislamu kwani walidai ameidhalilisha Qurani Tukufu.
2. Uhalifu wa Kuchomwa kwa makanisa ni moja ya utekelezwaji wa hotuba na maandishi ya wanaharakati (Fisabih Lilah) yanayowahimiza baadhi ya waislamu kudai haki zao za kutaka kujikomboa na Kanisa na Ukristo ambao wanadai ni matokeo ya ukoloni, na kwamba Tanzania inatawaliwa na mfumo wa Kikristo ambao umetapakaa kama damu mwilini kuanzia ngazi ya juu ya utawala wa nchi hadi chini kwa jina maarufu “MfumoKristo”(Tunao ushahidi wa hotuba na mafundisho ya wanaharakati katika CD, DVD na magazeti).
Inashangaza kuona serikali ambayo ndiyo yenye dhamana ya kusimamia ulinzi na usalama wa raia na mali zao; kupuuza madai haya na kushindwa kabisa kuzuia uhalifu wa matukio ya kuchomwa makanisa ambayo kimsingi ya nafanana kwani yalishatokea huko Zanzibar, Bagamoyo, Tunduru, Mwanza, Ndanda, Rufiji, Kigoma, Mto wa Mbu na sasa Mbagala;kwa kisingizio cha kuwaita wanaofanya matukio hayo kuwa ni wahuni.
Kwa kuwa ni wajibu wa serikali kuelekeza sera na shughuli zake zote katika lengo la kuhakikisha kwamba utu na haki nyinginezo zote za binadamu zina heshimiwa na kuthaminiwa, Baraza la Maaskofu wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania tungependa kuishauri Serikali yetu mambo yafuatayo:-
1. Irejee misingi ya Katiba yetu ya Jamhuri Ya Mungano waTanzania ambayo inatamka wazi kuwa; “Tanzania ni Nchi ya Kidemokrasia isiyokuwa na Dini”[KatibaYa 1977, Ibara ya 3 (1)].Hii itasaidia kuondoa hisia za kundi moja la Dini kuona idadi kubwa ya Viongozi na watawala waliopo madarakani pamoja na wakuu wa Vyombo vya ulinzi na usalama wako upande wadini Fulani.

2. Serikali kwa kushirikisha mabaraza yote ya kidini Nchini iundeTume huru itakayo kuwa najukumu la kusimamia na kuishauri serikali juu ya uendeshwaji wa shughuli za taasisi na jumuiya za kidini nchini. Jambo hili litasadia kubainisha mipaka ya kiutendaji kati ya uendeshwaji wa shughuli za kidini na mamlaka ya Nchi ambao umetajwa kwa wazi katika Katiba Ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ya 1977, ibara 19 (2);na hivyo kuondoa dhana ya kutaka kuingiza “udini” kwenye siasa ambayo inaelekea kuota mizizi Nchini.

3. Hata hivyo,baraza la makanisa ya Kipentekoste Tanzania tunatoa tamko kulaani uvunjifu waamani ambao umejitokeza kupitia vurugu zilizojitokeza hivi karibuni Nchini, na tuna waomba waumini wetu waendelee kudumisha hali ya utulivu na amani ambao umejengwa na waasisi wetu tangu Uhuru wa Nchi yetu; japo sote tunajua kuwa haki yetu ya kufanya ibada tuliyopewa na Mungu inaelekea kuvunjwa na watu wengine wasioheshimu uhuru wa ma wazo na imani katika dini. Nawafahamu kuwa yuko aliye juu kupita walio juu ambaye anayaona haya yote yanayotendeka.
Kwa ndugu zetu wanaoitwa Wanaharakati wa Kiisalamu, sisi tunajua imani yenu na mtazamo wenu kuhusu Wakristo; pamoja na msimamo mlionao juu ya kitabu cha Quran na juu ya kupigania Dini ya allah (subhahanahu wataa’alah); lakini kwa kuwa sote ni Watanzania tunawakumbusha kuwa jukumu la kudumisha amani ya Nchi yetu ni letu wote; hivyo, tutumie busara zetu katika kudumisha stahmala inayokazia kuheshimu hisia za watu wengine katika masuala ya kiimani kwani kutokufanya hivyo ni kuhalifu sheria tuliyojiwekea sisi wenyewe.
Aidha, Baraza la Makanisa ya Kipentekoste linaitaka serikali isisite kutoa tamko kali pindi vurugu za kidini zinapojitokeza bali iendelee kushughulikia migogoro ambayo inaweza kusababisha tena vurugu za kidini kwa nguvu zake zote, na iwabane waliohusika na uvunjajiwa makanisa warejeshe mali wakizochukua na kulipafidia za uharibifu wa kuchoma makanisa 10 Tanzania bara na jukwaa moja kwani kwa kufanya hivi itawahakikishia Watanzania kuwa hali hii haijitokez atena.Kwa matukio haya ya kuchomwa makanisa Nchini, Serikali yetu itambue kuwamacho na masikio ya wapenda amani Nchini na Ulimwenguni pote wanasubiri kwa hamu kuona ni hatua gani madhubuti serikali itachukua kwa watuhumiwa wa matukio ya uvunjwaji wa makanisa yaliyofanyika huko Zanzibar na Tanzania bara.
.............................. .............................. .......
Askofu Davidi Andulile Mwasota
Katibu Mkuu PCT Taifa.
MUNGU IBARIKI TANZANIA ILI IZIDI KUWA KISIWA CHA USALAMA NA AMANI.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top