Social Icons

Loading...

RAIS KIKWETE AWAONGOZA WAOMBOLEZAJI KUGA MWILI WA MAREHEMU JAJI GEORGE LIUNDI KARIMJEE DAR.

Rais Jakaya Kikwete, akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza
Rais Jakaya Kikwete, ameongoza viongozi wa Serikali na mamia ya waombolezaji kuaga mwili wa aliyekuwa msajili wa kwanza wa vyama vya siasa nchini, Jaji George Liundi, katika Viwanja vya Karimjee Dar es Salaam.
Mbali na Rais Kikwete viongozi wengine waliyoshiriki kuaga mwili wa Jaji Liundi ni Makamu wa Rais, Dk Mohammed Gharib na Rais mstaafu Benjamini Mkapa.
Wengine ni Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue na Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Ofisi ya vyama vya siasa iliwakilishwa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi, Msajili wa Vyama vya Siasa mstaafu, John Tendwa, Mawaziri, Mabalozi wa nchi mbalimbali pamoja na viongozi wa vyama vya siasa akiwamo Profesa Ibrahimu Lipumba wa Chama Cha Wananchi CUF na James Mbatia wa NCCR-Mageuzi.
Baada ya taratibu za kuaga mwili wa Jaji Liundi, alizikwa jana kwenye makaburi ya Chang’ombe Maduka Mawili ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadick aliongoza maziko hayo.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top