Social Icons

Loading...

MAJINA YA WABUNGE MAJANGILI SIRI KUBWA

Utata umeibuka kuhusu wabunge waliotajwa kwenye ripoti ya Kamati ndogo ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira kuwa wanahusika na biashara ya pembe za ndovu.
Wakati Ofisi ya Bunge ikidai kuwa ripoti hiyo haina majina ya wabunge, Mwenyekiti wa kamati hiyo, James Lembeli ameshikilia kuwa majina hayo ni sehemu ya ripoti hiyo ambayo baada ya kuwasilishwa, iliibua mjadala ambao ulisababisha mawaziri wanne kuong’oka.
Gazeti hili limedokezwa kuwa majina ya wabunge hao yalitajwa mbele ya kamati hiyo wakati ikichunguza jinsi Operesheni Tokomeza Ujangili ilivyotekelezwa, baada ya kuwapo kwa malalamiko ya vitendo vya ukatili na utesaji wa raia.
Hata hivyo, kwa mujibu wa taarifa hizo, wabunge hao hawakuitwa mbele ya kamati hiyo kuhojiwa kutokana na kwamba suala hilo halikuwa moja ya hadidu za rejea walizopewa kuzitafutia majawabu.
SOMA  ZAIDI:  http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Majina-ya-wabunge--majangili--siri-kubwa/-/1597296/2148976/-/tl4mhpz/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top