Rais alikuwa akirejea matukio ya hivi karibuni ya
marais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, Uganda, Yoweri Museveni na Rais wa
Rwanda, Paul Kagame kukutana na kujadiliana kuhusu masuala kadhaa
yanayohusu EAC bila Tanzania kuwapo.
“Hatuna mpango wa kuondoka, tupo na tunaendelea
kuwepo na napenda niwahakikishie kwamba Tanzania haijafanya jambo lolote
baya kwa jumuiya yetu au kwa nchi mwanachama mmoja mmoja na tumekuwa
waaminifu na watiifu kwa jumuiya wakati wote,”alisema Rais Kikwete.
Aliwashutumu viongozi wao akisema kuwa kauli zao
kwamba wanakutana kwa sababu wako tayari ni za kibaguzi kwani katika
mikutano yote waliyoifanya Entebbe nchini Uganda, Mombasa – Kenya na
Kigali nchini Rwanda hawakuwahi kuialika Tanzania.
“Hali hii haijawahi kuwapo na ni kwa mara ya
kwanza tunaanza kuwa na makundi ndani ya jumuiya yetu; huku Kenya,
Uganda na Rwanda, kule Tanzania na Burundi,”alisema Kikwete katika
hotuba yake iliyochukua saa1:15 na kuongeza:
“Ikiwa itakuja kutokea jumuiya ikadhoofika au
ikafa, Mungu apishilie mbali Tanzania isije ikanyooshewa kidole kwamba
ndiyo chanzo cha kudhoofika huko au kufa huko”.
Alisema ataendelea kuzungumza na viongozi wa nchi
hizo, na kwamba tayari ameanza ili kuhakikisha utekezaji wa mambo yote
ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unafanywa kwa kuzingatia mkataba
ulioanzisha jumuiya hiyo.Rais Kikwete alisema kwa mujibu wa mkataba huo
mambo yote yanapaswa kutekelezwa kwa kuzingatia kalenda ambayo inaweka
bayana mambo hayo kuwa ni Umoja wa Forodha, Soko la Pamoja, Umoja wa
Sarafu na hatimaye Shirikisho la Kisiasa.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/JK--Hatujitoi/-/1597296/2064458/-/jxdhd2/-/index.html
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/JK--Hatujitoi/-/1597296/2064458/-/jxdhd2/-/index.html
Post a Comment