Serikali imechukua uamuzi mgumu na kuamua kuwafariji wanafunzi 
waliofeli mitihani ya kuhitimu kidato cha nne mwaka 2012 baada ya kufuta
 matokeo hayo na kuamua yaandaliwe upya kwa kutumia utaratibu uliotumika
 mwaka 2011.
                
              
Uamuzi huo wa Serikali umetokana na matokeo mabaya
 ya mitihani huo yaliyosababisha zaidi ya asilimia 60 ya wanafunzi 
kupata sifuri.
Kutokana na matokeo hayo, Serikali iliunda Tume 
inayoongozwa na Profesa Sifuni Mchome kuchunguza matokeo hayo ili kupata
 ufumbuzi wa kudumu.
Muda mfupi baada ya tamko la Serikali, baadhi ya 
wadau wa elimu wameeleza kufurahishwa na uamuzi huo, huku Chama cha 
Walimu Tanzania (CWT) kikiikosoa hatua hiyo, kuwa imekiuka sheria na 
kupora madaraka ya Baraza la Mitihani Tanzania (Necta).
Akitoa kauli ya Serikali bungeni kuhusu taarifa ya
 awali ya Tume ya Taifa ya Kuchunguza Matokeo ya Mtihani wa Taifa Kidato
 cha nne mwaka 2012 jana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uratibu 
na Bunge), William Lukuvi alisema wameagiza Necta kuweka viwango ili 
matokeo ya wanafunzi yalingane na juhudi zao.
“Standardization ifanyike ili matokeo ya wanafunzi
 yalingane na juhudi wazizoziweka katika kusoma kwa mazingira, hali 
halisi ya Tanzania na uamuzi wa taifa kuongeza idadi ya shule na 
wanafunzi wakati uwekezaji katika ubora unaendelea,” alisema Lukuvi.
Chanzo http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1841582/-/12sx76v/-/index.html
Chanzo http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1841582/-/12sx76v/-/index.html





 
 
 
 
 
 
 
Post a Comment