Arusha. Lema aliyekamatwa usiku wa manane kuamkia 
Ijumaa wiki hii, alihojiwa kwa saa tatu mfululizo katika Kituo Kikuu cha
 Polisi, Arusha lakini alinyimwa dhamana kwa maelezo kwamba kuachiwa 
kwake kungehatarisha amani.
Akizungumza na gazeti hili kabla ya kujisalimisha 
kwa askari hao usiku huo wa kuamkia juzi, Lema alithibitisha kuwapo kwa 
polisi nje ya nyumba yake:
“Wapo nje ya nyumba yangu, wanatishia kupiga 
mabomu kama nisipotoka nje, lakini wanajadiliana na walinzi wangu na 
mimi nimewataka wanipe hati ya kunikamata,”alisema.
Wakili wa Lema, Humphrey Mtui alisema mahojiano ya
 mteja wake na polisi yalidumu kwa zaidi ya saa tatu kuanzia saa 7:50 
mchana hadi saa 11:15 jioni, na kwamba walitaka ufafanuzi kwenye hoja 
tatu walizodai kwamba zilijengwa kwenye kauli alizotoa Lema wakati 
alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa Taasisi ya Uhasibu Arusha (IAA).
Soma zaidi : http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760426/-/12b2syx/-/index.html
Soma zaidi : http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1760426/-/12b2syx/-/index.html





Post a Comment