Social Icons

Loading...

Waandishi wa habari wazuiwa Kamati za Bunge la Katiba Waandishi wa habari wazuiwa Kamati za Bunge la Katiba

Bunge Maalumu la Katiba limepitisha kanuni ya kuwazuia waandishi wa habari kuingia katika vikao vya kamati za chombo hicho, hatua ambayo inaelezwa ni kinyume na Katiba inayotoa uhuru wa wananchi kupata habari.
Kanuni hiyo ilipitishwa jana baada ya malumbano makali yaliyowagawa wajumbe wa bunge hilo, baadhi wakipinga kifungu hicho kwa sababu kinavunja Katiba ya nchi inayotoa uhuru kwa waandishi kukusanya na kusambaza habari na wengine wakiunga mkono kuwazuia.
Kanuni hiyo ilipitishwa kwa mbinde huku baadhi ya wajumbe wakiendelea kushikilia msimamo wa kuikataa, hata baada ya Mwenyekiti wa Muda wa bunge hilo, Pandu Ameir Kificho kuridhia kipite. Wajumbe waliopinga kanuni hiyo ni Joshua Nasari, Moses Machali, Peter Serukamba, Ezekiah Wenje na Maria Sarungi.
Baadhi ya wajumbe akiwamo Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kajubi Mukajanga walisimama kutaka kuzungumza lakini hawakupata fursa hiyo.
Mjumbe aliyekuwa mwiba kwa Tasnia ya Habari ni, Dk Harrison Mwakyembe ambaye aliwashawishi wajumbe kufunga mjadala huo ili wasonge mbele kwa madai kuwa hata yeye pia ni mwanahabari. “Hakuna upande usiotambua umuhimu wa vyombo vya habari katika mchakato huu... Tunachotofautiana ni jinsi na namna
ya ushiriki wa vyombo vya habari,” alisema Dk Mwakyembe. Alisema Taifa limeingia katika kipindi maalumu kama cha vita na kwa msingi huo, kanuni zinabadilika kulingana na mazingira na kwamba vyombo vya habari vinapaswa kulitambua hilo.
Soma  zaidi  http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Waandishi-wa-habari-wazuiwa/-/1597296/2234078/-/2npu1p/-/index.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top