Social Icons

Loading...

KIBONZO.... Matumizi ya Teknolojia IBADANI.

Sasa, Ibada zitakuwa kama ifuatavyo.
MCHUNGAJI: Bwana asifiweeeee!
WAUMINI: Ameeeeeeeeeni!
MCHUNGAJI: Tafadhalini washarika sasa tuchukue iPad,tablet PC, simu na kindle zetu ili tufungue 1 Wakorintho
13:13. Pia washeni bluetooth zenu ilimuweze kupokea mahubiri. Mnaotumia facebook, twitter, BBM na Whatsapp mnaweza kuendelea kupokea mahubiri haya. Washarika mnaweza kutumia Wi-Fi ya kanisa kwa uhuru kabisa.

WAUMINI: Haleluuuuyaaaaaaaah!
MCHUNGAJI: Wapendwa washarika sasa ni wakati wa sadaka kwa hiyo kadri ya itakavyokupendeza kumtolea
Mungu unaweza kutumia credit ama debit card, pia unaweza
kutoa sadaka kwa njia ya MPesa, Tigopesa, Airtel money
ama ZPesa kupitia namba zinazoonekana kwenye skrini.
WAKATI WA MATANGAZO
KATIBU WA USHARIKA: Wapendwa washarika wiki hii kutakuwa na mikutano ya kiroho kupigia group letu la Facebook. Mada kuu itakuwa uponyaji wa kiroho kwenye ndoa. Washarika wote mnakaribishwa kushiriki.
Siku ya Alhamisi kutakuwa na mafundisho ya Biblia moja kwa moja kupitia Skype kuanzia saa moja jioni. Tafadhali msikose kushiriki. Pia mnaweza kuendelea kufuatilia ibada hii pamoja na mafundisho yote kutoka kwa mchungaji
kupitia akaunti yake ya Twitter.
Haleluyaaaaaah!
WAUMINI
: Ameeeeeen
MCHUNGAJI
: Bwana asifiweeeee!
WAUMINI: Ameeeeeeeeeni!
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top