Social Icons

Loading...

Liwalo na Liwe!Baada Ya Jeshi La Polisi Kumwaga Mboga, Kanisa Lamwaga Ugali Katika Issue Ya Dkt Ulimboka

 
Mch: Gwajima
Sintofahamu katika Sakata ya issue ya Dr. Ulimboka imechukua sura mpya Baada ya Siku ya Ijumaa Jeshi la Polisi kujitokeza kwenye vyombo vya habari na kueleza Kuwa Mtuhumiwa wa Sekeseke la kumkamata na Kumtesa Dr. Ulimboka amekamatwa baada ya kwenda katika kanisa la Ufufuo na Uzima lililo chini ya Mch. Gwajima, Mchungaji huyo wa Kanisa hilo amefunguka siku ya jana na kueleza kuwa “Joshua The Kenyan” hakuwahi kwenda kwenye Kanisa hilo na wala Kanisa halina Utaratibu wa Kuungama kwa kusema dhambi.
Taarifa zilizotolewa juzi na kuibua maswali katikati ya Jamii ya Watanzania hususan Wakristo waliozipokea taarifa hizo kuwa Mtuhumiwa huyo aliyefikishwa kizimbani siku ya Ijumaa Asubuhi Mr. Joshua Mulindi Kwa maelezo ya Kova anafanya kazi chini ya kundi la Gun Star lililo chini ya Mkuu wa Kundi hilo Bw. Silence kutoka Nchini Kenya Walikuwa Wamekodiwa kuja Tanzania na Kigogo Mmoja kuja nchini kwa kazi moja ya Kutoa uhai wa Dr. Ulimboka na zoezi hilo kushindikana, ndipo kijana huyo wa Kikenya alikwenda kunako kanisa la Pastor Gwajima na Kukiri kuhusika na sakata zima la Dr. Ulimboka.
Kamanda  Kova  akitoa maelezo  kuhusiana  na kukamatwa  kwa Joshua Mulindi

Siku Ya Jana Mch. Gwajima amefunguka na kuruka Kimanga kuhusu sakata hilo na kutaka Kanisa hilo lisihusishwe na Sakata la Dr. Ulimboka sababu huyo mtu mwenye jina la Joshua kutoka nchini Kenya hajawahi kutubu kwenye Kanisa hilo na kueleza kuwa Kanisa lake halina utaratibu wa Kuungama kwa Kusema dhambi za waumini kama ilivyo katika Makanisa mengine hususan RC (Kuungama).
Mch. Huyo ambaye anaamini ana mahasimu wengi katika Gospel ameenda mbali zaidi na kusema kama Mkenya huyo ameeleza hayo basi atakuwa ametumwa na baadhi ya Watu wasioitakia mema huduma hiyo maarufu kwa kurejesha Misukule hapa Tanzania.
Source : http://samsasali.blogspot.com/2012/07/liwalo-na-liwebaada-ya-jeshi-la-polisi.html
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!

Post a Comment

CodeNirvana
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top