Loading...
Home » Archives for November 2013
Kitaifa Dk Mvungi afariki dunia.
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk Sengondo Mvungi (61)
amefariki dunia katika Hospitali ya Millpark Netcare, Johanesburg,
Afrika Kusini.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana kutoka
Afrika Kusini na kuthibitishwa na Msemaji wa Hospitali ya Millpark,
Tebogo Nyembezi zinasema Dk Mvungi alifariki dunia jana mchana. “Ni
kweli tulimpokea mgonjwa huyo kutoka Tanzania na alifariki 6:00 mchana
(saa 7:00 kwa saa za Afrika Mashariki),”alisema Nyembezi.
Nyembezi alisema kwamba walimpokea mgonjwa huyo
akiwa na majeraha ya kichwa, lakini aliahidi kueleza sababu ya kifo
chake leo baada ya kuzungumza na madaktari waliokuwa wakimtibu.Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji
Joseph Warioba pia alithibitisha kupokea taarifa za kifo hicho na kwamba
walikuwa wakiendelea kuandaa taratibu za kuleta mwili wake nchini.
“Ni pigo kubwa kwetu, tunaangalia namna ya
kuusafirisha kuja nchini na baadaye tutatoa taarifa rasmi,”alisema Jaji
Warioba na kuongeza:
“Kwa kweli ni pigo kubwa siyo kwetu tu, lakini
pigo kubwa kwa nchi yetu, tumepoteza mtu muhimu na kiungo muhimu sana.
Dk Mvungi, wengine tulimfahamu tangu alipokuwa mwanafunzi, alikuwa mtu
aliyesema kile alichokiamini, akikwambia kitu kilikuwa ni kile kilichopo
moyoni mwake”.
Soma zaidi : http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Dk-Mvungi--afariki-dunia/-/1597296/2070966/-/8ldfu2/-/index.html
Soma zaidi : http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Dk-Mvungi--afariki-dunia/-/1597296/2070966/-/8ldfu2/-/index.html
on Tuesday, November 12, 2013
JK: Hatutoki Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Rais Jakaya Kikwete amesema Tanzania haitajitoa katika Jumuiya
ya Afrika Mashariki (EAC), licha kuwapo kwa vitendo alivyoviita vya
ubaguzi vinavyofanywa na wakuu wa nchi za Uganda, Kenya na Rwanda.Rais Kikwete akilihutubia Bunge jana mjini Dodoma
alifichua kwamba sababu kubwa ya viongozi hao kuonekana kama wanaitenga
Tanzania ni msimamo wake kuhusu masuala ya Shirikisho la Kisiasa,
Uhamiaji, Ardhi na Ajira.
Rais alikuwa akirejea matukio ya hivi karibuni ya
marais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, Uganda, Yoweri Museveni na Rais wa
Rwanda, Paul Kagame kukutana na kujadiliana kuhusu masuala kadhaa
yanayohusu EAC bila Tanzania kuwapo.
“Hatuna mpango wa kuondoka, tupo na tunaendelea
kuwepo na napenda niwahakikishie kwamba Tanzania haijafanya jambo lolote
baya kwa jumuiya yetu au kwa nchi mwanachama mmoja mmoja na tumekuwa
waaminifu na watiifu kwa jumuiya wakati wote,”alisema Rais Kikwete.
Aliwashutumu viongozi wao akisema kuwa kauli zao
kwamba wanakutana kwa sababu wako tayari ni za kibaguzi kwani katika
mikutano yote waliyoifanya Entebbe nchini Uganda, Mombasa – Kenya na
Kigali nchini Rwanda hawakuwahi kuialika Tanzania.
“Hali hii haijawahi kuwapo na ni kwa mara ya
kwanza tunaanza kuwa na makundi ndani ya jumuiya yetu; huku Kenya,
Uganda na Rwanda, kule Tanzania na Burundi,”alisema Kikwete katika
hotuba yake iliyochukua saa1:15 na kuongeza:
“Ikiwa itakuja kutokea jumuiya ikadhoofika au
ikafa, Mungu apishilie mbali Tanzania isije ikanyooshewa kidole kwamba
ndiyo chanzo cha kudhoofika huko au kufa huko”.
Alisema ataendelea kuzungumza na viongozi wa nchi
hizo, na kwamba tayari ameanza ili kuhakikisha utekezaji wa mambo yote
ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki unafanywa kwa kuzingatia mkataba
ulioanzisha jumuiya hiyo.Rais Kikwete alisema kwa mujibu wa mkataba huo
mambo yote yanapaswa kutekelezwa kwa kuzingatia kalenda ambayo inaweka
bayana mambo hayo kuwa ni Umoja wa Forodha, Soko la Pamoja, Umoja wa
Sarafu na hatimaye Shirikisho la Kisiasa.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/JK--Hatujitoi/-/1597296/2064458/-/jxdhd2/-/index.html
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/JK--Hatujitoi/-/1597296/2064458/-/jxdhd2/-/index.html
on Thursday, November 7, 2013