Social Icons

Loading...

Champions League: Real Madrid humble Bayern Munich to reach final.

Real Madrid blew Bayern Munich away to reach the UEFA Champions League final with a 4-0 second leg victory which secured a 5-0 aggregate success.


NEMBO MAALUMU YA MIAKA 50 YA MUUNGANO


Kp Leo.


KIBONZO


CARS FOR SALE - AT A THROW AWAY PRICE

 TWO  CARS     FOR   SALE ...
 
 For  serious buyer pls  contact us  via  0784717342   or mail:audaxmujun@yahoo.com; 
 
1. A SUZUKI SWIFT   IN AN  IMACULATE  CONDITION.

REGISTERED RECENTLY (APRIL 2014)
YEAR:2004
CC:1320
PRICE: 7.5M NEGOTIABLE
 
 



 
 
 
=========================================================================== 
 
2. AN IST CAR (ATTACHED) IN AN IMACULATE CONDITION, AT A THROW AWAY PRICE. 
  REGISTERED RECENTLY (MARCH 2014)
YEAR:2004
CC:1300
PRICE: 9.5M  NEGOTIABLE
 
 



 
 
 
 FOR   SERIOUS  BUYER  KINDLY  CONTACT us via  0784717342
 
 mail:audaxmujun@yahoo.com; 
 
 
 
 

PLUIJM ,TAMBWE WAKAMIANA .


Kocha  wa Yanga, Hans van Pluijm na mshambuliaji wa Simba, Amis Tambwe kila moja amejigamba kuhakikisha klabu yake inamaliza msimu kwa kupata ushindi katika mchezo  wa mwisho baina ya timu hizo.
Kocha huyo Mholanzi ameipongeza Azam kwa kutwaa ubingwa na kusema waliweka changamoto na presha kubwa hasa katika mechi zao za mwisho ambazo wote walikuwa wakipambana bega kwa bega kuusaka ubingwa.
Pluijm alisema anaipongeza Azam kwa kutwaa ubingwa huo na kudai mechi tatu ziliwaharibia baada ya kutoka katika michuano ya kimataifa.
“Hatuwezi kulaumiana kwa sasa, tunawapongeza Azam kwa ubingwa, lakini uzembe wetu umetugharimu kwa kushindwa kutumia nafasi tuliyokuwa nayo hasa baada ya kutoka katika Ligi ya Mabingwa Afrika.
“Tulikuwa na michezo mingi mkononi kuliko wapinzani wetu, lakini tukashindwa kujipanga jambo ambalo lilitugharimu na kufanya tucheze kwa presha kubwa  mechi za mwishoni  ili kuusaka ubingwa, lakini tambua kila timu ilijipanga hivyo tunakubali matokeo,” alisema.
Pluijm alisema sasa hivi wanaangalia mechi yao ya mwisho dhidi ya Simba ili waweze kuibuka na ushindi na kujipanga kwa ajili ya msimu ujao na Kombe la Shirikisho.
“Tuko Moshi  leo (jana) tuna mechi  ya kirafiki na baada ya hapo tutarudi Dar es Salaam kuweka kambi kwa ajili ya mechi ya mwisho ya ligi dhidi ya Simba Jumamosi, naamini tutashinda mechi hiyo na mambo mengine yatafuata,” alisema Pluijm.
Naye mshambuliaji wa  Simba, Tambwe amekiri timu yao haikuwa vizuri msimu huu, lakini hawatakubali kamwe wafungwe na Yanga Jumamosi ili kuwafariji mashabiki wao.
Mrundi huyo Tambwe alisema hapingani na maneno ya mashabiki wengi kuwa timu yao haikuwa vizuri msimu huu na ndiyo maana imeshindwa kutwaa ubingwa wala nafasi ya pili, lakini amedai kuwa  mechi ya Jumamosi afe kipa afe beki ushindi lazima.
Test  
Today 

BUNGE LA KATIBA LAOMBA KUONGEZEWA SIKU 60

Bunge Maalumu la Katiba limeomba kuongezewa muda wa siku 60 kuanzia Agosti 5, mwaka huu litakapokutana kwa ngwe ya pili.
Bunge hilo linahitimisha ngwe yake ya kwanza Aprili 25, mwaka huu likiwa limekutana kwa siku 67, kati ya 70 zilizokuwa zimetengwa awali.

Kwa muda huo wa ziada 60, iwapo wajumbe wote 629 watalipwa posho ya Sh300,000 iliyopangwa kwa siku, jumla ya Sh11.322 bilioni za walipakodi zitatumika ukilinganisha na Sh13.209 bilioni zilizotumika katika siku 70 za awali. Jumla ya fedha zote zitakazotumika kwa posho ni Sh24.53 bilioni, bila kuingiza gharama nyingine nje ya posho za wajumbe.

Jana, Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta alitangaza kwamba shughuli za Bunge hilo zitakoma wakati wajumbe wake watakapokwenda kusherehekea maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano, Aprili 26, mwaka huu.

Sitta alisema jana kwamba aliwasilisha maombi ya kuongezewa muda kwa Rais Jakaya Kikwete, ambayo yalikuwa hayajajibiwa.

Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue alipoulizwa jana alisema: “Mheshimiwa Rais (Kikwete) anachoafiki ni kama ambavyo kila mtu anaona mwenendo wa Bunge ulivyo, kwamba siku 70 haziwatoshi, hivyo alikubali kwamba wanahitaji kuongezewa muda. Ingawa mpaka sasa hajaamua atawaongezea siku ngapi, atakapoamua tutawafahamisha tu.”

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema alisema upo uwezekano mkubwa wa Bunge hilo kuongezewa siku 60 lakini akaongeza kuwa hilo litategemea bajeti itakayoidhinishwa na Serikali.i 5.
chanzo  fungua  link 

KWA HERI WINDOWS XP

Kampuni ya utengenezaji wa mitambo endeshi ya kompyuta (Operating Systems) ya Microsoft ilisitisha utoaji wa huduma za muda mrefu kwa mitambo ya XP, ni moja ya mitambo endeshi inayotumika na watu wengi sana.Tangu kutoka kwa taarifa hizo, kumekuwa na maneno na mikanganyiko mingi mno kwa wateja hususan hapa Tanzania.

Kwakuwa ni mitambo inayotumika kwa weingi kwenye kompyuta nyingi zinazotumika kwenye mabenki na maofisini, hivyo watu walifika mbali hata kusema eti pesa zetu hazipo salama tena. Hivyo, ili kuondoa hofu hizi zinazoizunguka jamii, ungana nasi Dudumizi kwenye kujua nini maana ya kikomo hiki cha huduma na jinsi gani kinaweza kuathiri biashara yako?

 Kwanini XP imefikia kikomo?

XP iliingia sokoni miaka 12 iliyopita, tangu kuingia kwake, imekuwa ni mtambo endeshi unaotumika kwa wingi na makampuni mengi duniani kote. Na pia ni moja ya mtambo endeshi kutoka Microsoft uliokaa kwa muda mrefu sokoni. Ingawa katika uhai wa Windows XP, kumekuwa na matoleo mengine mengi kama Windows Vista, Windows 7 na ya sasa ambayo ni Windows 8, lakini kampuni ya Microfost imeendelea kutoka msaada wa kiufundi na kimatumizi kwa wateja wake wote, hivyo kwa maneno mengine tunaweza kusema,muda wake wa maisha umefika na ni mzigo kiutendaji na hata kibiashara kwa Microsoft kuendelea kuhudumia Windows XP ndiyo maana wameamua kusitisha huduma kwa Windows XP.

Je nini maana ya usisitshwaji wa Huduma?

Hapa ndipo palitokea mkanganyiko miongoni mwa watu wengi, kusitishwa kwa huduma hakumaanishi kuwa kompyuta zote zinazotumia XP hazitotumika tena kama wengine walivyoifananaisha na uhamaji wa mitambo ya analog kwenda Digital. 

Kusitisha kwa huduma kwa XP kunamaanisha, kampuni ya Microfot haitoendelea kutoa huduma (Support) kwa watumiaji wa windows XP tena, huduma hizi ni kama masasisho (updates) ya kiusalama, maboresho ya ufanyaji kazi (kama vile XP SP1, 2..) na huduma nyongine za utumiaji.

Hivyo, unaweza kuendelea kuitumia XP bila shida kama una uhakika kukosa huduma hizo hakutoathiri biashara.

Je kama ninatumia Windows XP, kompyuta yangu itaendelea kutumika?
Jibu ni ndiyo ila kuwa makini. Kusitishwa kwa huduma kwa Windows XP hakumaanishi kuondolewa kwa XP toka kwenye kompyuta yako, bali ni kutoweza pata huduma, hivyo Windows iliyopo kwenye komputa yako itaendelea kutumika kama kawaida, ila kuanzia sasa uhakika wa usalama wako utaendelea kupungua siku hadi siku.
Chanzo  mtandao  wa  dudumizi

KIBONZO



SWALI? 
HAPA  NI  WAPI?  MVUA ZA  DAR  ZINAZOENDELEA  KUNYESHA  ....

MVUA ZALETA MAAFA DAR ES SALAAM.

Vifo, uharibifu wa mali, miundombinu na mafuriko, msongamano wa magari, baadhi ya wakazi wa jiji hilo kukimbia makazi yao, wengine kulala kwenye magari na nyumba za wageni vimewakumba wakazi wa Jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake, kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha kwa siku ya nne mfululizo. 
  
Sehemu ya barabara iliyoharibika katika Daraja la Mpiji kwenye barabara ya Dar es Salaam Bagamoyo

Timu ya waandishi wa gazeti hili walifanya uchunguzi maeneo mbalimbali na kushuhudia hali halisi ilivyo, huku wanawake na watoto wakionekana kupata shida zaidi kwa kukaa nje ya nyumba zao, wengine kuhamia kwenye majengo ya shule.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam alisema jana kuwa walikuwa wakiendelea kukusanya taarifa za maafa ikiwamo vifo alivyosema ni vingi.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik alisema kuwa yupo kwenye kikao na watatoa taarifa zaidi za maafa baadaye.

Kijana ambaye akufahamika jina lake akijaribu kuokoa maisha ya akina mama waliotaka kusombwa na mafuriko jijini Dar es salaam
 
Tegeta, Boko na Bunju
Mtoto anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka minne, amefariki dunia baada ya nyumba aliyokuwa akiishi kujaa maji na kushindwa kujiokoa kutokana na ulemavu, wakati mama yake akiwa kwenye shughuli za biashara.
Majirani wa mtoto huyo walisema tofauti na kawaida yao kumtoa mtoto huyo mvua inaponyesha, jana walimsahau na mama yake aliporejea alikuta maiti ya mtoto wake ikielea chumbani.
Katika mvua hizo takribani kaya 180 zimekumbwa na mafuriko huku wakazi wake wakijikuta hawana pa kwenda.
“Mimi nimekuwa hapa tangu Tanu imezaliwa, nyumba yangu imejaa maji nimeshazeeka sina mtu wa kunisaidia, wala sijui wapi nitakwenda. Nomba Serikali inisaidie,”alisema Hussein Ngaoma ambaye ni mjumbe wa nyumba kumi katika eneo hilo.
Naye Husna Ally ambaye pia nyumba yake imekumbwa na mafuriko alisema: “Nasikitika, maana nimepata hasara kubwa. Mimi ni mfanyabiashara katika eneo hili la Boko, nina duka la kuuzia samani limejaa maji na sijaweza kuokoa chochote. Mzigo wa Sh30 milioni umeharibika wote.”
Jeti Lumo
Katika eneo hilo licha ya kujaa maji, mfanyabiashara ndogondogo amefariki dunia kwa kusombwa na maji 

   Uukoaji  ukiendelea  .

MDAU TOBI SHAURI MSHWAHILY APATA JIKO

Mdau   wa    blog na  forums   ya  JIACHIE    Mr  Tobi  Shauri   atimiza    ndoto  yake  muhimu  sana  ya  kupata  Jiko   , pichani  akiwa  na  mkewe  Bi  Angela   Tobi, kwa  niaba ya  blog  hii  nawatakia  KHERI  na  MAFANIKIO katika  maisha  yao  mapya  na mwanzo  mpya katika kila  jambo  mbele yao.

KP LEO


RAIS KIKWETE AWA BORA AFRIKA

Rais Jakaya Kikwete amechaguliwa kuwa kiongozi mwenye mchango mkubwa zaidi katika maendeleo barani Afrika kwa mwaka 2013.
Heshima hiyo kwa Rais Kikwete imetolewa na jarida la kimataifa la African Leadership Magazine Group na tuzo yake ilitarajiwa kutolewa jana jioni katika sherehe iliyopangwa kufanyika kwenye Hoteli ya St.Regis, Washington D.C, Marekani.
Taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu ilisema kuwa tuzo hiyo ilitarajiwa kupokewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe kwa niaba ya Rais Kikwete.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, tuzo hiyo hutolewa kwa viongozi wa Afrika ambao hutoa mchango mkubwa wa kiuchumi na kijamii kila mwaka kwa watu wao, kama ilivyokuwa kwa Rais Kikwete kutokana na mwelekeo wake wenye mafanikio kwa masuala ya utawala bora.
Taarifa hiyo ilisema kuwa jarida hilo limetambua utawala bora chini ya uongozi wa Rais Kikwete ambao limesema umeifanya Tanzania kuwa nchi ya kupigiwa mfano na kituo cha uhakika cha uwezeshaji kutokana na mageuzi yaliyofanywa katika sera na mifumo ya uchumi.
Ilisema kuwa, Rais Kikwete alikuwa chaguo la kwanza la wasomaji wa jarida hilo ambao walipiga kura kupitia njia mbalimbali za mawasiliano za jarida hilo.
“Kuhusu maoni ya wasomaji wetu juu ya kiongozi yupi wa Afrika ambaye ni hodari zaidi kwa maendeleo ya kiuchumi na maendeleo, matokeo ya majibu ya swali hilo yamedhihirisha bila shaka yoyote kuhusu nafasi ya Rais Kikwete katika uongozi wa nchi yake,” taarifa ya Ikulu imelinukuu jarida hilo na kuongeza: “Ushahidi uko kila mahali, ameweza kusimamia uchumi ambao umekuwa kwa wastani wa asilimia saba kwa miaka yote ya uongozi wake.”
Chanzo  gazeti  la  mwananchi.

HII NI KWELI ...


UEFA CHAMPIONS LEAGUE MADRID YAILAZA BVB 3- 0, CHELSEA YALALA 3-1 KWA PSG

MADRID  3     BVB  0


PSG 3    CHELSEA  1



Taarifa   zaidi    soma  hapa
uefa champions issues

UTAFITI : WATANZANIA WENGI BADO TUNATUNZA FEDHA NYUMBANI .

Asilimia 70 ya Watanzania wanatunza fedha zao nyumbani badala ya mfumo rasmi ukiwamo benki na huduma nyingine za fedha, imebainika.
Hayo yamebainishwa kwenye ripoti ya FinScope iliyotolewa jana na Mfuko wa Kuendeleza Huduma za Fedha Tanzania (FSDT), ikionyesha kuwa benki nchini zimeongezeka na kufikia 50.

Utafiti huo uliohusisha watu 8,000 umeonyesha kuwa asilimia 70.4 ya Watanzania milioni 24.2 wanaostahili kupata huduma za fedha, hawazitumii kutokana na sababu mbalimbali.

Sababu hizo ni pamoja na ukosefu wa elimu ya masuala ya fedha, umbali kufikia matawi ya benki au wakala, gharama kubwa za uendeshaji wa huduma hizo, mazoea ya mfumo wa kijima wa utunzaji wa fedha, kukosa imani kuhusu usalama wa fedha zao.

Akizindua ripoti hiyo, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu alisema jana kuwa pamoja na hali hiyo, kumekuwa na maendeleo makubwa katika sekta hiyo ukilinganisha na hali ilivyokuwa miaka minne iliyopita.
Soma  zaidi  mwananchi .

Man U Vs BM , Barca Vs Atletico Madrid mechi sare.

Man  U   1      Bayern   Munchen   1



Atletico  Madrid   1    Barca  1     


KIBONZO


KP Leo


Sauti za wananchi wa Dar kuhusu tatizo la foleni

Kwa wakazi wa Dar es Salaam, moja ya kero kubwa ni kukithiri kwa foleni za magari barabarani.
Hakuna asiyeguswa na atizo hilo kutokana na ubovu wa miundombinu na kutokuwepo na miundombinu ya kisasa ya usafiri ikilinganishwa na ongezeko la watu.
Ni mkoa unaoongoza kwa watu kupoteza muda mwingi barabarani, kiasi cha kuzorotesha hata utendaji wa kila siku na kuathiri shughuli za uchumi ambazo ni muhimu kwa maendeleo ya nchi.
Tatizo hili la foleni linaelezewa na wataalamu kwamba husabisha matatizo mbalimbali ya kiafya, ikiwa ni pamoja na watu kupatwa na ugonjwa wa kurukwa akili. Kisa cha haya yote ni foleni hizo ambazo inaonekana wazi kuwa zimekosa mwarobaini wa uhakika.
Hata hivyo, kama sehemu mojawapo ya kukabiliana na tatizo hilo, Serikali inaendelea na mradi wa mabasi yaendayo kasi. Kukamilika kwa mradi huo kunaelezwa kuwa kutasaidia kwa kiasi kupunguza tatizo la foleni barabarani katika baadhi ya maeneo ambayo mradi huo umeyagusa.
Hata hivyo, baadhi ya wakosoaji wanasema kuwa kuwapo kwa mradi huo wa mabasi yaendayo kasi hakuwezi kusaidia moja kwa moja kuondoa tatizo hilo ambalo limeendelea kuongezeka kutokana na ongezeko kubwa la idadi ya watu na kupanuka kwa shughuli za kiuchumi.

Watatu wakamatwa wakidaiwa kuvuruga Bunge.

Bunge la Katiba jana lilianza kujadili Rasimu ya Katiba kwa misukosuko kwenye Kamati baada ya kuvamiwa na kundi la wanaharakati waliokuwa na mabango wakidai hati halisi ya Muungano yenye saini za Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Karume.
Msukosuko mwingine uliozikumba karibu kamati zote zinazoanza kujadili rasimu hiyo kwa kuanzia sura mbili zinazohusu Muungano – sura ya kwanza na ya sita na kuzua malumbano, ni maana ya maneno dola, shirikisho, muungano na nchi.
Wakati waandamanaji wenye mabango wakiishia mikononi mwa polisi, suala la Muungano lilitulizwa kwa kuitwa wanasheria kutoa tafsiri sahihi kwa kila neno.
Katika kamati zote, suala la muda wa kamati kujadili sura hizo mbili kwa siku mbili kila moja pia liliibua mjadala mkali, hadi kuwalazimisha baadhi ya wenyeviti wa kamati kuamua kumwandikia mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta kuomba muda uongezwe.
Hali hiyo imejitokeza Bunge hilo likiwa limeshakaa siku 40 kabla ya kuingia katika mjadala rasmi, baada ya kupoteza muda mwingi katika kutengeneza kanuni za uendeshaji wa chombo hicho.
http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Watatu-wakamatwa-wakidaiwa-kuvuruga-Bunge/-/1597296/2266274/-/tg1uauz/-/index.html
© Copyright Daniel Blog in Contemporary News
Back To Top