Loading...
Home » Archives for August 2013
JK ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KIFO CHA ASKOFU DR KULOLA.
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
Fax: 255-22-2113425 |
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho
Kikwete ameshtushwa na kuhuzunishwa na taarifa za kifo cha Kiongozi wa
Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Askofu
Mkuu Moses Kulola ambaye ameaga dunia , Alhamisi, Agosti 29, 2013
katika Hospitali ya AMI iliyoko Masaki mjini Dar Es Salaam akiwa na umri
wa miaka 84.
Rais
kikwete ameelezea mshtuko na huzuni yake katika Salamu za Rambirambi
alizomtumia Katibu Mkuu wa Kanisa hilo Bwana Brown Mwakipesile kufuatia
kifo cha Askofu Mkuu Kulola.
“Nimeshtushwa,
nimesikitishwa na kuhuzunishwa sana na taarifa za kifo cha Mtumishi wa
Mungu wa muda mrefu na Askofu Mkuu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies
of God Tanzania (EAGT), Marehemu Moses Kulola kutokana na maradhi
yaliyomfanya wakati fulani apelekwe hadi India kupatiwa matibabu” amesema Rais Kikwete.
Rais
Kikwete amesema alimfahamu Marehemu Askofu Moses Kulola kwa miaka mingi
wakati wa enzi za uhai wake, kama Mtumishi Hodari wa Kiroho aliyejitoa
vilivyo katika kuwahudumia Waumini wa Kanisa lake ambapo mahubiri yake
yametoa mchango mkubwa katika kuimarisha imani za Waumini wake na
kusaidia kwa kiasi kikubwa katika kudumisha amani na utulivu wa nchi
yetu.
Aidha
Rais Kikwete amesema kifo cha Askofu Mkuu, Moses Kulola kimeacha pengo
kubwa siyo tu kwa Waumini wa Kanisa lake hapa nchini, bali pia miongoni
mwa wapenda amani kote nchini na kwingineko duniani kwa vile enzi za
uhai wake, Marehemu aliweza kufikisha ujumbe muhimu wa kiimani kupitia
mahubiri yake kwa watu wa mataifa mbalimbali ndani na nje ya Bara la
Afrika.
“Kwa
niaba yangu mwenyewe na Serikali ninayoingoza, ninakutumia wewe Katibu
Mkuu wa Kanisa la Evangelical Assembies of God Tanzania, Bwana Brown
Mwakipesile na Waumini wote wa Kanisa hilo Salamu za Rambirambi kutoka
dhati ya moyo wangu kwa kumpoteza Kiongozi muhimu wa Kiroho.
Ninawajulisha kuwa niko nanyi katika wakati huu mgumu kwa sababu msiba
wenu ni msiba wetu pia. Sala na mioyo yetu iko nanyi wakati wa
maombolezo ya kifo cha Kiongozi huyo shupavu wa dini. Nawaomba wote muwe
wavumilivu na wenye subira kwani yote ni Mapenzi yake Mola”, amesema Rais Kikwete.
“Vilevile
kupitia kwako, naomba unifikishie Salamu zangu za Rambirambi na pole
nyingi kwa familia, ndugu na jamaa wa Marehemu, Askofu Mkuu, Moses
Kulola kwa kumpoteza Baba, Kiongozi Shupavu na Mhimili wa familia.
Natambua fika kwamba hiki ni kipindi kigumu sana kwao cha maombolezo.
Natambua machungu yenu wakati huu na naungana nanyi katika kumwomba
Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aiweke peponi roho ya Marehemu Moses
Kulowa. Amina.”
Mazishi ya Marehemu, Askofu Mkuu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) yatafanyika
mjini Mwanza Jumatano ijayo tarehe 4 Septemba, 2013. Heshima za mwisho
kwa mwili wa Kiongozi huyo zitatolewa siku ya Jumamosi tarehe 31
Agosti, 2013 katika Kanisa laEAGT karibu na Hospitali ya Temeke kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 6.00 mchana.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
29 Agosti, 2013
on
ASKOFU Dr: KOLOLA AFARIKI
Askofu Mkuu wa Evangelistic Assemblies God Tanzania, Dr.Moses Kulola amefariki dunia
leo tarehe 28/08/2013 katika hospital ya AMI (African Medical Investments) iliyopo
Slipway jijini Dar es Salaam.
Askofu ana watoto wengi wa kiroho nchini Tanzania, Kanisa linahuzinishwa na habari
hizi, Bwana awape faraja kwa kipindi hiki, "Kuishi ni Kristo na kufa ni faida"
Jina la Bwana libarikiwe.
on
LUKUVI: Wabunge wengi wamo orodha ya dawa za kulevya.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge),
William Lukuvi amesema baadhi ya majina ya wabunge yametajwa miongoni
mwa watu wanaoshukiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya lakini
Serikali haiwezi kuwataja hadharani kwa haraka.
Majibu hayo ya Waziri Lukuvi yamekuja baada ya
wabunge kumbana na wengine wakizomea baada ya kueleza ugumu wa kutaja
majina ya washukiwa pasi na ushahidi wa kutosha.
“Serikali haiwezi kutaja majina haraka kiasi hicho
kwani inaogopa kukurupuka na kushindwa mahakamani, hivyo lazima tuwe
makini sana na jambo hilo. Hatuwezi kukurupuka tu eti ni fulani wakati
hatuna vithibitisho.
“Kumbukeni wengine mpo humu ndani ya Bunge na
tukianza wengi mtakwisha maana katika orodha hiyo kubwa na ninyi mmo na
orodha ni kubwa kweli ambayo wakati mwingine inatakiwa umakini wa hali
ya juu,” alisema Lukuvi alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa
Karatu (Chadema), Mchungaji Israel Natse.Katika swali lake ambalo lilisababisha kelele za
kuzomea, Natse alitaka majina hayo yatajwe hadharani. Hata hivyo, hali
ilitulia baada ya Spika wa Bunge, Anne Makinda kuingilia kati na kusema:
“Hii tabia ya zomeazomea siitaki humu ndani, acheni tabia hiyo lazima
mumsikilize mtu kwa kile anachokisema kwanza lakini mtindo huu si
mzuri...”
Patashika hiyo ilitokana na swali la Mbunge wa
Viti Maalumu (CCM), Catherine Magige aliyetaka kujua iwapo Serikali
inaweza kuwaambia Watanzania ukubwa wa biashara hiyo nchini na kama
haioni kama kuna tatizo katika ukaguzi wa abiria na mizigo katika
viwanja vya ndege na juhudi za Serikali kumaliza tatizo hilo.
Akijibu swali hilo, Lukuvi alisema ukubwa wa
biashara hiyo hapa nchini unadhihirishwa na idadi ya Watanzania 274
waliokamatwa kati ya mwaka 2008 hadi Julai mwaka huu kwa kosa la
kujihusisha na dawa za kulevya katika nchi mbalimbali za nje.
Alisema Serikali inafahamu ukubwa wa tatizo la
matumizi ya biashara hiyo haramu ya dawa za kulevya nchini na alitaja
takwimu za ukamataji wa dawa hizo katika kipindi cha kuanzia mwaka 2000
hadi Machi, 2012.
Alisema pamoja na kukamatwa kwa Watanzania hao nje
ya nchi, wageni 31 wanashikiliwa mahabusu katika Magereza ya Keko na
Ukonga, Dar es Salaam ambao ni raia wa Iran, Pakistan, Senegal na Afrika
Kusini.
Hata hivyo, katika swali lake la nyongeza, Magige
alisema uteketezaji wa dawa zinazotajwa kukamatwa umekuwa wa siri kiasi
cha kutiliwa shaka kuwa huenda zinachukuliwa na maofisa waliozikamata
ndiyo maana hakuna uwazi.
Chanzo: mwananchi
Chanzo: mwananchi
on Tuesday, August 27, 2013
UDSM: No taking back students who sued us.
Students
who filed a law suit against the University of Dar es Salaam have not
being allowed back but seven of their counterparts who did not go to
court and also offered official apologies have been permitted to resume
classes in the academic year of 2013/2014.
This development adds to the on going saga that was sparked last year when the university’s management expelled 15 students and suspended 86 others for boycotting classes demanding 43 of their expelled colleagues be unconditionally reinstated.
But instead of rescuing their class mates, they too were expelled and the university ahas refused to allow them back short of an apology, several behavioural reports from their immediate supervisors and for those who seeked justice through the court system, they are not to return to class until the courts gives its ruling.
“…those who provided the reports and offered official apologies will resume classes but those who went to court will remain expelled because we cant intervene the court proceeding” said the University Deputy vice Chancellor (administration) Prof. Yunus Mgaya during an exclusive interview held yesterday in Dar es Salaam.
Among them were leaders of the students’ organization (Daruso) which include the speaker, Minister for Education and Academics Deputy Minister.
Earlier in January 2012, 15 students were expelled, apparently only seven offered apologies and received the clean reports from the Dean of students, the relevant Academic units and also official recognition from their District Administration recognising who they are and their residency.
Prof. Mgaya, a Marine Biology professor, made it clear that the University would not tolerate any behaviour that breaches their codes of conduct and threaten the campuses peace and tranquility in any way or form.
Affirming that the institute will not reinstate the students who filed the law suit to contest their expulsion, Prof. Mgaya remained adamant that they will not receive any leniency short of the court proceeding running their due course and then also for the students to provide the required behaviour reports.
“…what the university wants is for the students to provide behaviour reports from the Dean of students, heads of their various Academic units and also from their local government district officials as to authenticate their residency and communal profiles,” he asserted.
As for the seven who resume class following their apologies, the professor had this to say: “We will prepare conditions for them to meet. They will have to make sue they don’t breach our conditions otherwise they are out,”
He maintained that both continuing and incoming students must keep a peaceful environment to ensure education and other activities conducted by the university continue to run smoothly. As implicated by the don, any who would, for a reason or another, derail from this norm will be faced with stringent repercussions and that includes expulsion.
This development adds to the on going saga that was sparked last year when the university’s management expelled 15 students and suspended 86 others for boycotting classes demanding 43 of their expelled colleagues be unconditionally reinstated.
But instead of rescuing their class mates, they too were expelled and the university ahas refused to allow them back short of an apology, several behavioural reports from their immediate supervisors and for those who seeked justice through the court system, they are not to return to class until the courts gives its ruling.
“…those who provided the reports and offered official apologies will resume classes but those who went to court will remain expelled because we cant intervene the court proceeding” said the University Deputy vice Chancellor (administration) Prof. Yunus Mgaya during an exclusive interview held yesterday in Dar es Salaam.
Among them were leaders of the students’ organization (Daruso) which include the speaker, Minister for Education and Academics Deputy Minister.
Earlier in January 2012, 15 students were expelled, apparently only seven offered apologies and received the clean reports from the Dean of students, the relevant Academic units and also official recognition from their District Administration recognising who they are and their residency.
Prof. Mgaya, a Marine Biology professor, made it clear that the University would not tolerate any behaviour that breaches their codes of conduct and threaten the campuses peace and tranquility in any way or form.
Affirming that the institute will not reinstate the students who filed the law suit to contest their expulsion, Prof. Mgaya remained adamant that they will not receive any leniency short of the court proceeding running their due course and then also for the students to provide the required behaviour reports.
“…what the university wants is for the students to provide behaviour reports from the Dean of students, heads of their various Academic units and also from their local government district officials as to authenticate their residency and communal profiles,” he asserted.
As for the seven who resume class following their apologies, the professor had this to say: “We will prepare conditions for them to meet. They will have to make sue they don’t breach our conditions otherwise they are out,”
He maintained that both continuing and incoming students must keep a peaceful environment to ensure education and other activities conducted by the university continue to run smoothly. As implicated by the don, any who would, for a reason or another, derail from this norm will be faced with stringent repercussions and that includes expulsion.
SOURCE:
THE GUARDIAN
on
JK ataka vyuo vikuu nchini kudahili wanafunzi wengi.
Rais Jakaya Kikwete amevitaka vyuo vikuu nchini kuweka nguvu
zaidi, kuhakikisha vinadahili wanafunzi wa shahada za juu ili kupata
wahadhiri.
Akizungumza baada ya kutoa hati idhini kwa Vyuo
Vikuu na Vyuo Vikuu Vishiriki vinane, Rais Kikwete alisema kufanya hivyo
vitakabiliana na tatizo la uhaba wa wahadhiri linalovikabili hivi sasa.
“Pale kwenye upungufu tusisite kutafuta wataalamu
wengine kutoka nje ya nchi. Wakati wa miaka ya 1970 tulipokuwa tunasoma
pale Chuo Kikuu (Mlimani), tulikuwa na wahadhiri wengi kutoka nje,”
alisema Rais Kikwete.Licha ya suala hilo, Rais Kikwete alisisitiza umuhimu wa vyuo hivyo kuwekeza kwenye utoaji elimu bora.“Ikumbukwe idadi kubwa ya wanafunzi haitoshi,
lazima tuzingatie ubora. Tunataka mwanafunzi anayepata shahada nchini
ajulikane popote anapokwenda,” alisema Rais Kikwete na kuongeza
Taarifa kwa hisani ya mwananchi.
Taarifa kwa hisani ya mwananchi.
on Tuesday, August 20, 2013
CAG apewa maagizo ya kukagua ufisadi wa bil 13.
Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali Kuu (PAC), imeiagiza
ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi
maalumu wa matumizi ya Sh13 bilioni, katika Mkutano wa Benki ya
Maendeleo Afrika (ADB) uliofanyika Mei mwaka 2012.
Uamuzi huo umekuja baada ya kubainika kwa matumizi
mabaya ya fedha hizo, yaliyofanywa na Hazina kwa ajili ya ununuzi wa
samani za ofisini na kompyuta ndogo 200.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Zitto Kabwe alisema
mbali na vituo hivyo, Hazina pia imenunua, seti za televisheni za
ukutani, mashine za kuchapishia karatasi, viti na makochi ya sebuleni.
Alisema ingawa vifaa hivyo vimenunuliwa kwa fedha
za Serikali, baadhi yake vimeachwa katika ukumbi wa Kituo cha Mikutano
cha Kimataifa cha Arusha, bila ya kuwapo kwa makabidhiano ya kisheria.
“Kamati imepata mashaka kuhusu matumizi ya Sh13
bilioni katika mkutano wa ADB, jambo lililotufanya tumuombe CAG kufanya
ukaguzi maalumu wa matumizi ya fedha hizi za Serikali,” alisema Zitto.
zaidi soma
zaidi soma
on
Huyu ndiye Trafiki Feki aliyekamatwa.
kwa habari zaidi gonga
http://issamichuzi.blogspot.com/2013/08/update-mambo-yalivyokuwa-baada-ya.html
http://issamichuzi.blogspot.com/2013/08/update-mambo-yalivyokuwa-baada-ya.html
on Sunday, August 18, 2013
Dr Mwakyembe aahidi kula sahani moja na wauza UNGA.
Siku moja baada ya kufanya ziara ya ghafla Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison
Mwakyembe amesema leo ataweka hadharani majina ya watu wanaosafirisha
dawa za kulevya nchini.
Dk Mwakyembe juzi alifanya ziara hiyo JNIA kukagua
utendaji kazi kwenye uwanja huo ikiwa ni siku chache baada ya kutokea
kashfa ya kupitishwa kwa dawa za kulevya na baadhi ya Watanzania
wakiwamo wasanii kukamatwa sehemu mbalimbali duniani.
Aidha, hatua ya waziri huyo imekuja siku tatu
baada ya ahadi aliyotoa akiwa Mwanza kwamba katika kipindi cha wiki
mbili kuanzia juzi, atahakikisha anawakamata vigogo wote walio katika
mtandao wa usafirishaji na uingizaji wa dawa za kulevya kupitia viwanja
vyote vya ndege nchini.
Akihutubia katika maadhimisho ya Siku ya Kimataifa
ya Vijana iliyoandaliwa na Taasisi ya Jitambue Foundation,
yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Nyamagana, Dk Mwakyembe alisema yuko
tayari kufa katika vita hivyo.
Akizungumza na Waandishi wa Habari ofisini kwake
jana, Dk Mwakyembe alisema: “Kesho (leo) nitawataja wanaojihusisha na
dawa za kulevya. Kwa sasa nakamilisha ushahidi wa kutosha ikiwa ni
pamoja na picha za wahusika.”
Aliwaonyesha waandishi wa habari picha ya
mtuhumiwa mmoja ambaye alisema alikamatwa saa nane baada ya waziri huyo
kufanya ziara uwanjani hapo. “Ninataka watu wafahamu wanaoliingiza taifa
hili katika aibu hii, ambayo inasababisha Watanzania wasiaminike katika
viwanja vya ndege vya mataifa mengine.”
“Hatuwezi kuwa taifa la kuogopaogopa, hii ni vita
ya kusafisha nchi yetu, kwani ni nani mwenye mkataba na Mungu kuwa
ataishi milele?” alihoji Waziri huyo alipokuwa akijibu swali kuwa suala
la kuwataja watu wanaowafichua wasafirisha unga linaweza likaweka rehani
maisha yake.
“Kama hupendi joto usiingie jikoni”, alisema.
Akizungumzia watendaji wa JNIA kuhusiana na dawa
za kulevya, alisema: “Mfanyakazi yeyote atakayebainika kuhusika
kuwasaidia wasafirisha unga atafukuzwa kazi na ambaye atafanya juhudi ya
kuwakamata wasafirishaji hao atapewa zawadi.”
“Kuna watu wanadhani tunafanya mzaha katika jambo
hili. Jana baada ya mimi kuondoka usiku wa saa 2:30 huyu (kijana
aliyekamatwa) akaingia na mzigo,” alisema Dk Mwakyembe na kuongeza kuwa
alikamatwa na kete 86 za dawa aina ya heroini na misokoto 34 ya bangi
aliyokuwa akiisafirisha kwenda Italia kupitia Zurich.
Aliiagiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kuwatunuku wafanyakazi waliofanikisha kukamatwa kwa kijana huyo.
Akizungumzia hali ya Uwanja wa JNIA baada ya
kufanya ziara juzi, Dk Mwakyembe alisema tatizo halipo kwenye vitendea
kazi, bali wafanyakazi wasiokuwa waaminifu.
Chanzo gazeti la mwananchi.
Chanzo gazeti la mwananchi.
on
Dr. Ndalichako aichanachana Elimu ya Tanzania.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Nchini (Necta), Dk Joyce
Ndalichako amesema karatasi za majibu ambazo wamekuwa wakizipata kutoka
kwa wanafunzi zinaonyesha kuwa, watoto wengi wanahudhuria shuleni lakini
hakuna wanachojifunza.
Dk Ndalichako aliyasema hayo jana jijini hapa
alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa mabaraza ya mitihani ya Afrika,
ambao umejikita kujadili suala la tathimini ya elimu kwa nchi za Afrika.
Hii ni mara ya kwanza kwa Dk Ndalichako kuzungumza
tangu Serikali itangaze kufuta matokeo ya kidato cha nne mwaka 2012 na
kutaka yapangwe upya, suala ambalo lilipingwa na wadau wengi wa elimu.
Alisema kuwa wakati nchi nyingi za bara hili
zikiwa zimejitahidi kuongeza upatikanaji wa elimu kwa watu, ubora wa
elimu unaendelea kuwa tishio kwa watu wa bara hili kwa vizazi vijavyo.“Kama mabaraza ya mitihani, tumekuwa tukiona
karatasi za majibu kutoka kwa wanafunzi ambazo zinaonyesha kwa uwazi
kabisa kuwa watoto wanahudhuria shuleni lakini hakuna wanachojifunza,”
alisema Dk Ndalichako.
Chanzo gazeti la mwananchi
on
TAARIFA YA POLISI KUHUSU TUKIO LA SHEIHK PONDA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
DAR ES SALAAM AGOSTI 10, 2013.
1. MNAMO
TAREHE 10, AGOSTI ,2013 MAJIRA YA SAA 8 MCHANA, MAENEO YA SHULE YA
MSINGI KIWANJA CHA NDEGE MANISPAA YA MOROGORO, KULIFANYIKA KONGAMANO LA
BARAZA LA EID LILILOANDALIWA NA UMOJA WA WAHADHILI MKOANI MOROGORO.
DAKIKA KUMI KABLA YA KONGAMANO HILO KUMALIZIKA ALIFIKA SHEKHE PONDA
ISSA PONDA AMBAYE ALIZUNGUMZA KWA MUDA MFUPI.
2.
KONGAMANO HILO LILIFUNGWA MAJIRA YA SAA 12:05 JIONI AMBAPO WATU
WALIANZA KUTAWANYIKA, BAADHI YAO WAKIWA WAMEZINGIRA GARI DOGO ALILOKUWA
AMEPANDA SHEKHE PONDA. BAADA YA KUTOKA KATIKA ENEO HILO, ASKARI WA
JESHI LA POLISI WALIZUIA GARI HILO KWA MBELE KWA NIA YA KUTAKA KUMKAMATA
SHEKHE PONDA AMBAYE MPAKA SASA ANATUHUMIWA KWA KOSA LA KUTOA MANENO YA
UCHOCHEZI SEHEMU MBALIMBALI HAPA NCHINI YENYE MLENGO WA KUSABABISHA
UVUNJIVU WA AMANI.
3.
BAAADA YA ASKARI KUTAKA KUMKAMATA, WAFUASI WAKE WALIZUIA UKAMATAJI HUO
KWA KUWARUSHIA MAWE ASKARI. KUFUATIA PURUKUSHANI HIYO, ASKARI WALIPIGA
RISASI HEWANI KAMA ONYO LA KUWATAWANYA.
4.
KATIKA VURUGU HIZO, WAFUASI HAO WALIFANIKIWA KUMTOROSHA MTUHUMIWA. HIVI
SASA IMETHIBITIKA KUWA SHEKHE PONDA YUKO KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA
MUHIMBILI AKITIBIWA JERAHA KATIKA BEGA LA MKONO WA KULIA LINALODAIWA
ALILIPATA KATIKA PURUKUSHANI HIZO.
5.
KUFUATIA TUKIO HILO, TIMU INAYOSHIRIKISHA WAJUMBE KUTOKA JUKWAA LA HAKI
JINAI IKIONGOZWA NA KAMISHINA WA JESHI LA POLISI CP ISSAYA MNGULU
IMEANZA KUFANYA UCHUNGUZI WA TUKIO HILO.
6. AIDHA, JESHI LA POLISI LINATOA WITO KWA WANANCHI KUWA WATULIVU WAKATI SUALA HILI LINASHUGHULIKIWA KISHERIA.
Imetolewa na:-
Advera Senso- SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
on Sunday, August 11, 2013
Jomo Kenyatta airport closed after major fire.
A
major fire at Jomo Kenyatta International Airport (JKIA) has forced
authorities to close it as fire crews attempt to put it out, kenya's
airport authority says.No reports of casualities have been established yet and the actual cause of the Wednesday morning fire remains unclear.Kenya Airways tweeted: Esteemed Guests, JKIA is closed due to the
unfortunate fire incident, all flights cancelled please don't come until
we update soon.Images posted on Twitter and local TV show smoke and flames gushing from one of the main buildings.
Kenya Airports Authority (KAA) confirmed that the airport would be closed and passengers evacuated.
The airport authority sent out a statement confirming "reports of a fire at JKIA affecting part of [the] international arrivals building and Unit 1 departures.
"KAA Fire and Rescue Team is on [the] ground being assisted by G4S and Nairobi Fire Brigade. Passengers have been evacuated to safety."
One of the local media, Citizen TV, posted on Twitter that fire engines were "running dangerously low on water. Please give way to bowsers ferrying water to the airport".
The fire at east Africa's busiest airport started at around 5.00am local time (EAT) in the immigration section of the departure lounge and spread to the international arrivals area, a Kenya Civil Aviation Authority official said on condition of anonymity.
Source: http://www.newvision.co.ug/news/645819-jomo-kenyatta-airport-closed-after-major-fire.html
Kenya Airports Authority (KAA) confirmed that the airport would be closed and passengers evacuated.
The airport authority sent out a statement confirming "reports of a fire at JKIA affecting part of [the] international arrivals building and Unit 1 departures.
"KAA Fire and Rescue Team is on [the] ground being assisted by G4S and Nairobi Fire Brigade. Passengers have been evacuated to safety."
One of the local media, Citizen TV, posted on Twitter that fire engines were "running dangerously low on water. Please give way to bowsers ferrying water to the airport".
The fire at east Africa's busiest airport started at around 5.00am local time (EAT) in the immigration section of the departure lounge and spread to the international arrivals area, a Kenya Civil Aviation Authority official said on condition of anonymity.
Source: http://www.newvision.co.ug/news/645819-jomo-kenyatta-airport-closed-after-major-fire.html
on Tuesday, August 6, 2013
FAHAMU Salim Kikeke wa BBC wapi kapitia hadi kufika pale alipo.
Mtangazaji wa idhaa ya kiswahili BBC Ndg Salim Kikeke. |
Licha ya kauli hii ya Dk Dyneer, kuna vijana wengi
nchini wanaonekana wamekata tamaa; Wengine hufikiri kwamba kama
umezaliwa katika familia duni, maana yake utakuwa na maisha duni milele,
huku wale ambao wamezaliwa katika familia tajiri, wanafikiri
wataendelea kuwa tajiri.Hata hivyo ukweli ni kwamba mtu yeyote anaweza
kuwa na maisha bora, kama anavyosema msomi Hope Clark katika kitabu
chake Fedha za Waandishi cha hivi karibuni nchini Ireland, kwamba siri
ya kufanikiwa katika maisha ni kuishi kwa malengo, kuishi vizuri na watu
na kupenda kuwa karibu na wasiokata tamaa.
Mwalimu Julius Nyerere wakati fulani amewahi
kunukuliwa akisema ‘Uchumi mnao, mmeukalia’. Kila mtu alitafsiri
alivyoweza, lakini ukweli hasa ni kwamba mtu yeyote akijipanga vizuri
kwa maana ya kutuliza akili yake, kukaa na watu wa kumshauri vizuri na
kufanyia kazi mambo au mipango anayoipanga, anaweza kufanikiwa
anachotaka...Ni ukweli kuwa kuna wengi wana maisha duni kwa sababu
pamoja na mambo mengine ya tabia zao za kukata tamaa, waoga wa
kuthubutu.
Kati ya vijana ambao wanaonekana kupambana hadi
kuweza kujenga majina na heshima zao Duniani ni Salim Kikeke; Ni mtu
ambaye kama angekata tamaa hakika asingefika aliko sasa.
Sasa amekuwa ni mtu wa kujadiliwa na umaarufu wake
hauko tu Tanzania, bali maeneo mengi ya Dunia hasa kunakozungumzwa
Kiswahili. Huyu mtu ni kati ya watangazaji wakongwe na kivutio cha watu
wengi kutoka barani Afrika na duniani kote, lakini katokea wapi?
Taarifa kamili bofya kikeke
Taarifa kamili bofya kikeke
on
AMBAVYO WENGER HATOMSAHAU DROGBA ALIYEKATAA KUMSAINI KWA PAUNI 100,00 TU AKIWA KINDA TENA UFARANSA
KAMA Arsene Wenger alihitaji ukumbusho
wowote wa kosa alilofanya katika usajili akiwa kazini Arsenal, Didier
Drogba alifanya hivyo Uwanja wa Emirates Jumapili.
Mabao mawili ya Drogba ya dakika za lala
salama dhidi ya Arsenal yaliyowezesha Galatasaray kubeba Kombe la
Emirates yameendeleza rekodi ya mshambuliaji huyo dhidi ya The Gunners
na kufika mabao 15 katika mechi 15.
Kwamba, katika dakika 1175 ambazo Drogba
amecheza dhidi ya Arsenal, amefunga wastani wa bao moja katika kila
dakika 78 na sekunde 20.
Ulikuwa usiku wa pigo kwa Wenger, ambaye alikataa kumsajili Drogba kwa Pauni 100,000.
Akiwa anachipukia nyota huyo wa Ivory
Coast katika miaka yake minne Le Mans kati ya mwaka 1998 na 2002, jicho
la skauti wa Wenger lilimnasa mchezaji huyo.
Wenger alikataa kumsajili, na Drogba akahamia timu nyingine ya Ligue 1, Guingamp akiwa ana umri wa miaka 23 kwa Pauni 80,000.
Wenger alisema mwaka 2009:
"Tumemuangalia kwa umakini alipokuwa Le Mans. Siyo sisi tu
tuliomuangalia. Lakini tulifikiri hawezi tayari kiasi cha kutosha.
"Lilikuwa ni kosa, lakini ukiwa kwenye
soka, kila mmoja anaweza kuelewa. Tulikuwa na Thierry Henry. Tulisema
tutafuatilia maendeleo ya Drogba. Hatukuwahi kumkataa,"
Mwaka 2004, kufuatia msimu wa mafanikio makubwa akiwa Marseille, Drogba alisaini Chelsea kwa ada ya Pauni Milioni 24.
Kana kwamba hilo halikuwa pigo tosha katika jino la Wenger, Drogba aliifanyizia ile mbaya timu yake uwanjani.Alifunga mabao 13 katika mechi 14 dhidi ya Arsenal enzi zake akiwa Stamford Bridge, mengi kati yao akifunga katika mechi muhimu.
Wenger alipata ahueni wakati Drogba
alipoondoka Chelsea kuhamia Shanghai Shenhua mwaka jana, akisema wakati
huo: "Sijui ni kiasi gani Chelsea wamempoteza, lakini hatumkumbuki.
Amefanya madhara mengi dhidi yetu katika kila mechi,".
Drogba anaweza kuwa ukingoni mwa soka
yake akiwa na umri wa miaka 35 sasa, lakini kwa Emirates atabakia
kukumbukwa kama kiboko ya timu ya Wenger hadi siku atakapotungika daluga
zake.
Mfaransa huyo sasa atakuwa anaomba dua
Arsenal isipagwe kundi moja na Galatasaray katika Ligi ya Mabingwa
katika droo inayotarajiwa kupangwa mjini Monaco Agosti 29.
Taarifa na picha kwa hisani ya bin Zubeiry.
Taarifa na picha kwa hisani ya bin Zubeiry.
on
Tanzanian relations with Rwanda in 'difficult'.
Relations between Tanzania and neighbour Rwanda are strained,
Tanzanian President Jakaya Kikwete has acknowledged against a backdrop
of conflict in eastern Democratic Republic of Congo.
"Since the end of May, our relations with Rwanda have gone through difficult times," Kikwete said in a frank speech to the nation late Friday, criticising "statements by the leaders of Rwanda against myself and against our country".
At an African Union summit meeting in Ethiopia in May, Kikwete advised Rwanda, Uganda and DR Congo to open negotiations with rebel forces.
But in response, Kigali angrily suggested that Kikwete was speaking for the Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR), a Rwandan Hutu rebel group based in DR Congo.
"The relationship (with Rwanda) became difficult after my advice to the Rwandan government to talk to his opponents," said Kikwete, speaking in Swahili.
"I gave the same advice to the governments of Congo and Uganda," Kikwete added.
Tanzania has sent troops to join the UN peacekeeping force in eastern DR Congo, taking part in a special brigade to target multiple rebel forces there, including the FDLR as well as the M23, a mainly Tutsi group founded last year.
UN experts have accused Kigali of backing M23 fighters, claims that Rwanda strongly denies.
But Kikwete said he wanted to ensure "good relations" with Kigali.
"I would like to reiterate that I and the Tanzanian government have no bad intentions against Rwanda," Kikwete said.
Some accuse Tanzania of being close to the Rwandan opposition in exile, including Colonel Patrick Karegeya, Kigali's former intelligence chief now based in South Africa.
Karegeya and former army chief of staff Faustin Kayumba Nyamwasa, also exiled in South Africa, formed the opposition Rwanda National Congress three years ago, which calls for their former comrade President Paul Kagame to step down.
source : http://www.globalpost.com/dispatch/news/afp/130804/tanzanian-relations-rwanda-difficult
"Since the end of May, our relations with Rwanda have gone through difficult times," Kikwete said in a frank speech to the nation late Friday, criticising "statements by the leaders of Rwanda against myself and against our country".
At an African Union summit meeting in Ethiopia in May, Kikwete advised Rwanda, Uganda and DR Congo to open negotiations with rebel forces.
But in response, Kigali angrily suggested that Kikwete was speaking for the Democratic Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR), a Rwandan Hutu rebel group based in DR Congo.
"The relationship (with Rwanda) became difficult after my advice to the Rwandan government to talk to his opponents," said Kikwete, speaking in Swahili.
"I gave the same advice to the governments of Congo and Uganda," Kikwete added.
Tanzania has sent troops to join the UN peacekeeping force in eastern DR Congo, taking part in a special brigade to target multiple rebel forces there, including the FDLR as well as the M23, a mainly Tutsi group founded last year.
UN experts have accused Kigali of backing M23 fighters, claims that Rwanda strongly denies.
But Kikwete said he wanted to ensure "good relations" with Kigali.
"I would like to reiterate that I and the Tanzanian government have no bad intentions against Rwanda," Kikwete said.
Some accuse Tanzania of being close to the Rwandan opposition in exile, including Colonel Patrick Karegeya, Kigali's former intelligence chief now based in South Africa.
Karegeya and former army chief of staff Faustin Kayumba Nyamwasa, also exiled in South Africa, formed the opposition Rwanda National Congress three years ago, which calls for their former comrade President Paul Kagame to step down.
source : http://www.globalpost.com/dispatch/news/afp/130804/tanzanian-relations-rwanda-difficult
on Sunday, August 4, 2013
Rais Clinton atua nchini
Rais wa Mstaafu wa Marekani, Bill Clinton jana alifanya ziara
katika makazi ya watu duni eneo la Vingunguti, wilayani Ilala Dar es
Salaam, ambapo alikagua miradi midogomidogo ya wananchi inayofadhiliwa
na mfuko wake (Bill Clinton Foundation).
Clinton alitembelea eneo hilo akitokea moja kwa
moja Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam
(JNIA), alipowasili akiwa katika ziara ya nchi mbalimbali za Afrika
kukagua miradi inayoendeshwa na mfuko wake.
Katika eneo hilo rais huyo mstaafu alipokewa kwa
shamrashamra mbalimbali ikiwamo ngoma za kiasili huku baadhi ya wananchi
wakipigwa butwaa na kutoamini macho yao kwa kiongozi huyo kutembelea
makazi yao.
Aidha, Clinton alipata wasaa wa kusalimiana na
wakazi wa Vingunguti wakiwamo watoto ambao walishindwa kuzuia hisia zao
wakijaribu kumsogelea, hali iliyomsukuma Clinton kuwasogelea na
kuwasalimia kwa kuwashika mikono.
Maneno ya ‘Welcome Vingunguti Clinton‘ yalisisika
kutoka kwa wananchi kuashiria kumkaribisha rais huyo wa 42 wa Marekani
wakati alipowasalimia akitumia takriban dakika 15.
Clinton alikagua miradi ya midogomodogo ya
wananchi iliyo chini ya mfuko wake ikiratibiwa na kutekelezwa na Shirika
la Kimataifa la Kuhudumia Watoto (Plan) pamoja na Benki ya Barclays
kupitia Vikoba.
Miradi aliyokagua ni pamoja na saluni za kinamama,
ushonaji na chips ambapo pia alishuhudia mmoja wa wanachama wa vikundi
hivyo akikabidhiwa mkopo wa Sh100,000 ambaye alieleza mbele ya Clinton
kuwa atazitumia kwa mradi wa maandazi, hali iliyomfanya rais huyo na
umati wa watu uliohudhuria kucheka.
Akizungumza katika ziara hiyo Clinton alizishauri
benki nchini, kuwekeza kwenye vikundi vya kuweka na kukopa (Vikoba)
akieleza kuwa ndiyo mkombozi kwa wananchi hasa wanawake.
“Nimekuwa kwenye miradi hii kwa miaka 30 kabla
sijawa rais, hivyo basi najua umuhimu wake. Benki zinatakiwa zisaidie
Vikoba kwani vikundi hivyo huwafikia wananchi kwa haraka na wepesi hivyo
basi kunahitajika njia mbadala za kuhakikisha vinakuwa imara,” alisema
Clinton na kuongeza;
“ Raha ya maendeleo ni kuona watu wanajitegemea wenyewe katika shughuli za kujiingizia kipato.”
Mmoja wa wananchi walionufaika, Zainab Paul ambaye
ni mwanachama wa Kikundi cha Amani Hisa alisema kuwa kupitia Mfuko wa
Bill Clinton na Vikoba ameweza kujikwamua kimaisha ikiwamo kumlipa mtoto
wake karo ya shule.
“Kikundi chetu kina wanachama 30 na huwa tunanunua
hisa kwa Sh2000 na kila mwanachama anaruhusiwa kukopa zaidi ya mara
tatu,” alisema Paul.
Chanzo Mwananchi
Chanzo Mwananchi
on